taifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Sat, 18 Jul 2026 06:27:44
Chama chazinduliwa kulinda haki za wafanyakazi katika miradi ya kilimo
CHAMA kipya cha kitaaluma kimezinduliwa nchini ili kuimarisha ulinzi wa haki za kibinadamu za wafanyakazi na jamii zinazoathiriwa kwenye miradi ya kilimo na maendeleo, wasiwasi ukishamiri kuhusu ukiukaji wa haki za wafanyakazi, migogoro ya ardhi na ulegevu wa ulinzi wa kijamii. Social Impact Management Association of Kenya (SIMAK), ni muungano utakaowakutanisha wataalamu wanaohakikisha miradi ya maendeleo, hususan katika kilimo na miundombinu, inazingatia haki za kibinadamu na kushirikisha jamii zinazoathirika. Kaimu Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Edward Ontita, akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi jijini Nairobi alisema lengo ni kuhakikisha kila mradi mkubwa unakuwa na maafisa wa usimamizi wa kijamii kuanzia hatua ya kupanga hadi kukamilika. "Tunataka viwango endelevu vizingatiwe katika miradi yote ya maendeleo. Maendeleo yanawahusu watu, hivyo haki zao lazima zilindwe," akasema. [caption id="attachment_190228" align="aligncenter" width="300"] Kaimu Mwenyekiti wa Social Impact Management Association of Kenya (SIMAK), Profesa Edward Ontita (kulia) akikabidhi mmoja wa wanachama wa muungano huo cheti cha kuwa memba. Picha|Sammy Waweru[/caption] Prof Ontita alisema mashamba makubwa ya kilimo ni miongoni mwa sekta zilizoathirika zaidi na ukatili wa kijinsia, unyanyasaji wa kingono, mishahara duni na mazingira mabaya ya kazi. "Baadhi ya wafanyakazi hulipwa chini ya kiwango cha chini cha mshahara kilichowekwa kisheria, huku wengine wakikosa maji safi, vyoo bora na uhuru wa kujiunga na vyama vya wafanyakazi. Hizi ni haki za msingi za binadamu," alisema. Aliongeza kuwa jamii zinapaswa kushirikishwa kuanzia hatua za kwanza, hasa katika miradi inayohusisha ununuzi wa ardhi na ulipaji wa fidia. Aidha, alisema miradi ya mikopo ya kaboni na uhifadhi wa bioanuwai inapaswa kushirikisha wananchi kikamilifu ili wanufaike. "Kutofuata masharti ya ulinzi wa kijamii husababisha ucheleweshaji wa miradi na hasara ambazo tumefanya hesabu zinafika Sh600 bilioni" Ontita alionya. [caption id="attachment_190230" align="aligncenter" width="300"] Kaimu Mwenyekiti wa Social Impact Management Association of Kenya (SIMAK), Profesa Edward Ontita wakati wa mahojiano jijini Nairobi mnamo Juni 26, 2026. Picha|Sammy Waweru[/caption] Kwa upande wake, Kaimu Karani katika Idara ya Maendeleo ya Jamii katika Wizara ya Ulinzi wa Jamii na Masuala ya Wazee, Dkt Lynett Ochuma, alisema serikali inaandaa sera ya kitaifa ya kusimamia hatari zinazokumba jamii ili kuoanisha sekta hiyo na viwango vya kimataifa huku ikizingatia mazingira ya wafanyakazi nchini Kenya. Alisema sera hiyo itashughulikia haki za wafanyakazi, afya na usalama wa jamii, kuzuia unyanyasaji wa kingono, kulinda makundi yaliyotengwa na kuhakikisha ununuzi wa ardhi na uhamishaji wa watu unafanyika kwa haki. "Ushirikishwaji wa wadau ni msingi wa maendeleo. Maendeleo hayapaswi kudhuru jamii bali yanapaswa kuwa jumuishi," alisema, akiongeza kuwa sera hiyo itawasilishwa bungeni kama mswada baada ya kukamilika.
read morestandardmedia.co.ke
@standard Sat, 18 Jul 2026 04:19:29
President Ruto's official website down in second suspected hack within a year
President William Rutos official website, president.go.ke, was down on Saturday after hackers allegedly took control of the homepage and replaced it with a ransom message.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Sat, 18 Jul 2026 06:16:19
Daphne van Domselaar Siblings: Get to Know Naomi van Domselaar
Daphne van Domselaar is a Dutch professional footballer born on March 6, 2000, in Beverwijk, Netherlands. She plays as a goalkeeper for Arsenal in the Womens Super League and is a key member of the Netherlands womens national team. She is known for her commanding presence in goal, strong shot-stopping abilities, distribution skills, and composure [...] The post Daphne van Domselaar Siblings: Get to Know Naomi van Domselaar appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Sat, 18 Jul 2026 06:22:24
Emily Fox Siblings: Meet Alex and Leslie Fox
Emily Ann Fox is an American professional soccer player born on July 5, 1998, in Ashburn, Virginia. She plays primarily as a right-back for Arsenal in the Womens Super League and for the United States womens national team. Fox is renowned for her exceptional speed, technical ability, defensive solidity, and versatility across the backline. She [...] The post Emily Fox Siblings: Meet Alex and Leslie Fox appeared first on Kahawatungu.
read morekenyanews.go.ke
@kna Sat, 18 Jul 2026 05:03:30
Murkomen says public participation key to security reforms
Interior and National Administration Cabinet Secretary Kipchumba Murkomen has reaffirmed the importance of public participation in strengthening governance, saying meaningful citizen engagement is essential in shaping reforms and safeguarding constitutional democracy. Speaking at the Trans Nzoia County Assembly in Kitale during the opening of the County Assembly Wellness and Committee Services Centre, Murkomen said public...
read morekenyanews.go.ke
@kna Sat, 18 Jul 2026 05:07:05
Directorate reviews of public- private partnerships policy
The Directorate of Public-Private Partnerships (PPP), domiciled at the National Treasury and Economic Planning, has kicked off public participation forums to ensure community engagement, transparency, and stakeholder buy-in of its activities. The PPP Directorate is the technical arm of the PPP Committee at the National Treasury, mandated to facilitate, structure and manage infrastructure and development...
read morekenyanews.go.ke
@kna Sat, 18 Jul 2026 05:11:37
West Pokot Set to host KICOSCA and KYISA Games
West Pokot County has set in motion preparations to host two of Kenyas biggest inter-county sporting events after delegates from across the country expressed satisfaction with the countys state of preparedness following a four-day inspection tour of sports facilities and accommodation venues. The delegation, comprising officials from the Kenya Inter-County Sports and Cultural Association (KICOSCA)...
read morekenyanews.go.ke
@kna Sat, 18 Jul 2026 05:15:54
Coastal residents urged to back government development agenda
Cabinet Secretaries Salim Mvurya (Youth Affairs, Creative Economy and Sports) and Hassan Joho (Mining, Blue Economy and Maritime Affairs) are actively urging residents in the coastal region to support the national development agenda. The two leaders emphasized the importance of community collaboration with the national government in driving sustainable economic activity, job creation, and the...
read moreRight Column Content