taifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Wed, 22 Jul 2026 00:55:35
Mwanamume aliyepatwa amemeza mihadarati alazimishwa kuitema
POLISI katika Kaunti ya Mombasa wanamzuilia mwanamume aliyepatikana amemeza madonge ya dawa za kulevya, akilenga kuyasafirisha hadi Dubai yakiwa ndani ya mwili wake. Mnamo Julai 15, wakati wasafiri wakisubiri kuabiri ndege ya saa saba mchana kutoka Mombasa kuelekea Dubai, wapelelezi katika Uwanja wa Kimataifa wa Moi jijini Mombasa walikuwa wakimfuatilia mwanamume huyo mwenye umri wa miaka 67. Taarifa za kijasusi zilikuwa zimemhusisha na mtandao wa kimataifa wa biashara ya dawa za kulevya, huku wachunguzi wakishuku kwamba alikuwa ameficha kokeini ndani ya mwili wake. Wapelelezi kutoka Kitengo cha Kupambana na Dawa za Kulevya cha Idara ya Kuchunguza Uhalifu (DCI), wakishirikiana na maafisa wa usalama wa uwanja huo wa ndege, walimkamata kabla ya kuabiri ndege. Operesheni hiyo baadaye ilihusishwa na mtandao wa kimataifa wa biashara ya dawa za kulevya ambao umekuwa ukichunguzwa kwa miezi kadhaa. [caption id="attachment_190364" align="alignnone" width="2560"] Polisi wapata mihadarati kutoka kwa msafiri mmoja aliyekuwa anaelekea Dubai Picha|Kevin Odit[/caption] Walanguzi hao wa kimataifa hutumia Mombasa kama kituo cha kupitisha dawa za kulevya kuelekea nchi nyingine za nje. Mshukiwa alikamatwa na kupelekwa katika kituo maalumu cha kutengwa kwa ajili ya uangalizi wa kimatibabu. Baadaye alipelekwa katika Hospitali ya Port Reitz, ambapo madaktari na wahudumu wa afya walimweka chini ya uangalizi wa karibu ili kusaidia kutoa dawa hizo alizokuwa amemeza kwa njia salama. Polisi walisema wataalamu wa matibabu walifanikiwa kutoa vidonge 44 vilivyofunikwa kutoka tumboni mwake kwa njia iliyolenga kuvizuia kupasuka. "Dawa hizo za kulevya zitatumika kama vielelezo mahakamani," alisema Kamanda wa Polisi wa eneo la Pwani Ali Nuno. Kulingana na wachunguzi, kumeza dawa za kulevya ili kukwepa ukaguzi wa usalama ni mojawapo ya njia hatari zaidi za kusafirisha dawa hizo, kwa sababu vikipasuka ndani ya mwili vinaweza kusababisha maafa. Polisi walifichua kwamba kukamatwa kwa mwanamume huyo kulitokana na operesheni inayoendelea ambayo hadi sasa imesababisha kukamatwa kwa washukiwa wengine kadhaa, wakiwemo wanaodaiwa kuwa walanguzi wakuu wa dawa za kulevya. Kwa jumla, dawa za kulevya zenye thamani ya karibu Sh151 milioni zimepatikana na polisi katika kipindi cha karibu miezi minne iliyopita. Operesheni hiyo pia ilifanikisha kukamatwa kwa mshukiwa mwingine ambaye wapelelezi wanaamini alikuwa kinara wa biashara hiyo haramu. Wakati wakiendeleza uchunguzi, maafisa walivamia nyumba iliyoshukiwa kutumiwa kama maficho na kituo cha muda cha kuwahifadhi wasafirishaji wa dawa za kulevya. Upekuzi huo ulisababisha kupatikana kwa vipande vingine 16 vinavyodhaniwa kuwa na kokeini. Uchunguzi unaendelea kubaini ukubwa kamili wa mtandao huo na kuwatambua washukiwa wengine. Takwimu zilizotolewa na Kitengo cha Kupambana na Dawa za Kulevya cha DCI zinaonyesha kwamba wapelelezi wamekamata kilo 37 za heroini zenye thamani ya takriban Sh111.846 milioni katika miezi minne iliyopita. Pia wamekamata gramu 1,336 za kokeini zenye thamani ya takriban Sh5.344 milioni. "Jumla ya watu tuliowakamata kuhusiana na dawa za kulevya ni washukiwa 27. Kati yao, watano ni wafanyabiashara wakubwa wa dawa za kulevya bila shaka yoyote, 10 ni wasafirishaji na 12 ni wauzaji," alisema Bw Nuno. Ripoti hiyo pia inaonyesha kwamba maafisa walikamata gramu 204 za methamphetamine, inayofahamika zaidi kama meth, yenye thamani ya takriban Sh1.632 milioni katika operesheni zilizofanywa katika kipindi cha miezi minne iliyopita. Bangi bado ndiyo dawa ya kulevya inayokamatwa zaidi katika eneo hilo, polisi wakiripoti kukamata kilo 10,747.84 zenye thamani ya takriban Sh32.243 milioni katika kipindi hicho. Kwa jumla, thamani ya dawa zote za kulevya zilizokamatwa katika operesheni za kupambana na biashara hiyo katika eneo la Pwani ni takriban Sh151.065 milioni.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Wed, 22 Jul 2026 00:21:38
Maude Apatow Net Worth
Maude Apatow is an American actress who has a net worth of $2 million. She is best known for playing Lexi Howard on the HBO teen drama series Euphoria. Apatow began acting as a child, appearing in films directed by her father, filmmaker and comedian Judd Apatow, often alongside her mother, actress Leslie Mann. Over [...] The post Maude Apatow Net Worth appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Wed, 22 Jul 2026 00:25:59
Decomposed body of unidentified man found in bush in Nyandarua
Police in Nyandarua County are investigating murder after the decomposed body of an unidentified man was discovered in a bush near Ol Kalou Township. The body was found on Tuesday afternoon in the Kanyamwe area after a member of the public alerted authorities. Police visited the scene and confirmed the incident. Police said the body, [...] The post Decomposed body of unidentified man found in bush in Nyandarua appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Wed, 22 Jul 2026 00:40:12
Three workers killed in caretaker attack in Kiambu Town
Three casual workers were killed after a suspected former caretaker allegedly attacked them while they slept at a residential compound in Kiambu Town on Tuesday morning. Police said the incident occurred at a property along Mukumo Drive off Njadhaini Road belonging to a woman, who is reportedly out of the country. According to preliminary investigations, [...] The post Three workers killed in caretaker attack in Kiambu Town appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Tue, 21 Jul 2026 23:56:59
Chrissy Teigen Net Worth
Chrissy Teigen is an American model, television personality, author, and entrepreneur who has an estimated net worth of $100 million. The figure represents the combined wealth of Teigen and her husband, musician and producer John Legend, with Legend contributing a significant share of the couples fortune. However, Teigen has also built a successful career and [...] The post Chrissy Teigen Net Worth appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Wed, 22 Jul 2026 00:05:56
Kate Upton Net Worth
Kate Upton is an American swimsuit model and actress who has an estimated net worth of $20 million. Upton rose to international fame after becoming a prominent Sports Illustrated Swimsuit model and appearing on the publications cover several times. Her modeling career also included appearances in major international editions of Vogue, Harpers Bazaar, GQ, Cosmopolitan, [...] The post Kate Upton Net Worth appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Wed, 22 Jul 2026 00:14:30
Leslie Mann Net Worth
Leslie Mann net worth is estimated at $160 million, a figure that represents the combined wealth she shares with her husband, filmmaker Judd Apatow. Mann has built a successful career as an actress and producer, while Apatow has earned significant wealth through his work as a director, writer and producer. Leslie Mann is best known [...] The post Leslie Mann Net Worth appeared first on Kahawatungu.
read moreRight Column Content