kenyanews.go.ke
@kna Mon, 06 Jul 2026 10:55:07
Kericho Housing Project Sparks MSME Growth Around Construction Site
The ongoing Affordable Housing Project in Kericho County has led to the offshoot of many accompanying small businesses around the construction site, creating numerous opportunities for local entrepreneurs and improving household incomes. The Majengo Talia Affordable Housing Programme (AHP), just a stone's throw away from the Kiprugut Chumo Stadium on the outskirts of Kericho Town,...
read morekenyans.co.ke
@kenyans Mon, 06 Jul 2026 11:52:47
Police Sound Warning Ahead of Planned Saba Saba Day March
Saba Saba in Kenya is one of the most iconic days in the country's history, marred by political unrest and observed as a national symbol of resistance and the fight for civic rights.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Sun, 05 Jul 2026 12:12:09
Kongamano la KAKAMA maadhimisho ya Kiswahili Burundi kutoa mwelekeo mpya
WANANCHI wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wametakiwa kushiriki kikamilifu ili kufikia malengo ya mwelekeo mpya ulioanzishwa na Kamisheni ya Kiswahili ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (KAKAMA) katika kuhakikisha akiliunde inatumika kuleta maendeleo ya Kiswahili. Kakama imeazimia kuanzisha mwelekeo huo mpya ili kuafikia mafanikio kupitia Kongamano la Kimataifa la Tatu ambalo linaanza kesho Jumapili Julai 5, 2026 na maadhimisho ya Siku Kiswahili Duniani Julai 7, ambapo kwa pamoja yanafanyika Bujumbura Burundi. Akizungumza na waandishi wa habari, jijini Bujumbura wikendi, Katibu Mtendaji wa Kakama, Dk Caroline Asiimwe alisema kila nchi wanachama zinatakiwa kushiriki kikamilifu ili kufikisha azma ya Kakama kuleta maendeleo ya Kiswahili katika teknolojia ya akiliunde pamoja wingi lugha kama inavyosema kaulimbiu ya mwaka huu. Amesema maeneo yanayotakiwa kutiliwa mkazo ni kwenye uwekezaji, ubunifu na ushirikiano. Bi Asimwe ametoa wito uwekezaji zaidi ufanyike kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo kampuni za kuzalisha maudhui ya Kiswahili kwa kutumia akiliunde, kubuni mifumo mbalimbali na kuongeza ushirikiano wa kibunifu wa kikanda. "Ninatoa wito kwa wana Afrika Mashariki kushiriki kwa namna mbalimbali ikiwemo kwenye uwekezaji, ubunifu na ushirikiano," akasisitiza Dk Asiimwe. Amesema watunga sera pia wanalojukumu kutumia fursa hiyo kwenye nchi wanachama kuhimiza sera zinazochochea matumizi ya teknolojia ya akili unde. Dk Asiimwe amewakaribisha wana Afrika Mashariki kutoka kada mbalimbali kushiriki kongamano hilo kwa namna mbalimbali ikiwemo kufika kwenye mkutano na kufuatilia mitandaoni. Amesema kongamano hilo linaenda sambamba na maadhimisho ya miaka 10 ya Kamisheni ya Kiswahili tangu kuazishwa kwake. Amewataka wanajumuiya ya Afrika Mashariki kujivunia mafanikio mbalimbali yaliyopatikana tangu kuanzishwa kwa kamisheni hiyo.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Sun, 05 Jul 2026 21:55:49
Zaheer kuhojiwa, Arati akijitetea kuhusu ghasia za Keumbu
GHASIA za Ijumaa dhidi ya msafara wa Linda Mwananchi katika Kaunti ya Kisii ambapo mtu mmoja aliuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa zinaonyesha jinsi ushindani wa kisiasa unavyoendelea kuzua uhasama huku uchaguzi mkuu wa 2027 ukikaribia. Idara ya polisi jana ilithibitisha kuwa maafisa wa usalama wamewakamata washukiwa saba na kuwahakikishia Wakenya kuwa msako wa kuwatafuta washukiwa wengine unaendelea. Tukio hilo limethibitisha kuwa baadhi ya viongozi wakuu wa kisiasa katika eneo la Gusii wanahusika katika kueneza na kufadhili uhuni wa kisiasa ili kusambaratisha mikutano ya wapinzani wao. Mbunge mmoja anayehudumu muhula wa kwanza akishirikiana na kiongozi mmoja wa ngazi ya kaunti wanahusishwa na kufadhili ghasia hizo zilizotokea eneo la Keumbu. Inadaiwa viongozi hao wawili waliwanunulia vijana mipini ya majembe, mapanga na silaha nyingine ili kuvamia mikutano ya Linda Mwananchi. Hapo jana, maafisa kutoka Idara ya Upelelezi (DCI) mjini Kisii walisema kuwa wamemwamrisha Mbunge wa Nyaribari Chache Zaheer Jhanda afike mbele yao ili ahojiwe kuhusu ghasia hizo zilizosababisha kifo cha mtu mmoja. "Mbunge Zaheer Jhanda, ameagizwa kufika katika afisi za DCI, Kaunti ya Kisii leo asubuhi kuhusiana na uchunguzi unaoendelea," ikasema taarifa ya Idara ya Polisi ikisisitiza kuwa wote waliovamia msafara wa Linda Wananchi watanyakwa na kufikishwa kortini. Vincent Osiemo 'Mapinduzi' aliaga dunia jana hospitalini. Alikufa kutokana na majeraha ya kuanguka kutoka kwenye gari lililokuwa likiendeshwa kwa kasi huku madereva wakikwepa mawe yaliyokuwa yakirushwa Keumbu. Marehemu alikuwa alikuwa katika kikosi cha wanahabari wanaofanyia kazi Linda Mwananchi. Taarifa hiyo ilitolewa baada ya wananchi kuonyesha hasira baada ya kusambaa kwa video zilizoonyesha polisi wakitembea sako kwa bako na watu waliodhaniwa kuwa wahuni waliokuwa wakiurushia mawe msafara wa Linda Mwananchi. Wabunge Clive Gesairo (Kitutu Masaba) na mwenzake wa Bomachoge Borabu, Obadiah Barongo, waliotangaza kifo cha kijana huyo, walishutumu vyombo vya usalama kwa kutoa silaha kwa makundi ya wahuni wa kisiasa. Wanasiasa hao wawili walithibitisha kuwa watu 20 walijeruhiwa kutokana na ghasia za eneo la Keumbu. Gavana wa Kisii, Simba Arati, naye amepinga madai kuwa alihusika kwa kufadhili wahuni dhidi ya viongozi wa Linda Mwananchi. Bila kutoa ushahidi wowote, gavana huyo alidai kuwa baada ya viongozi wa upinzani kumaliza mikutano yao, waliwaachilia "wahuni wao" waliowaleta Kisii kuwashambulia wananchi wasio na hatia, na hivyo kuwalazimu wakazi kujilinda. "Niliwaambia wafuasi wangu wasiingilie mkutano wa Linda Mwananchi. Baada ya kumaliza mikutano yao kwa amani, waliwaachilia wahuni wao waliowaleta Kisii na kuwalazimisha wananchi wajilinde dhidi ya wahuni hao," akasema Bw Arati mjini Ogembo. "Nawauliza watu wa Ogembo, mnaweza kutazama watu waje hapa waanzishe fujo bila kujitetea?" akauliza. Video zilionyesha wavamizi wakirusha mawe kwenye magari yaliyokuwa katika msafara wa viongozi wa upinzani. Madereva walikimbia kwa hofu huku baadhi ya wafuasi wakidondoka kutoka kwenye magari na kujeruhiwa vibaya. Kwenye video hiyo hakuna ushahidi unaoonyesha kuwa kulikuwa na makundi mawili yaliyokuwa yakipigana kama ilivyodaiwa na gavana pamoja na baadhi ya maafisa wa usalama wa Kisii. Wavamizi hao walionekana kuwa wamejipanga vizuri na walikuwa na silaha tayari kutekeleza uhalifu huo ulionekana ulipangwa mapema. Aliyekuwa Jaji Mkuu David Maraga, ambaye alijiunga na timu ya Linda Mwananchi Ijumaa, gari lake liliharibiwa katika vurugu hizo za kurushiana mawe. Naibu Kiongozi wa Chama cha Jubilee Dkt Fred Matiang'i, ambaye ngome yake ya kisiasa ni Kisii, alitaka Kamanda wa Polisi wa Kaunti ya Kisii afutwe kazi kutokana na kisa hicho. Mweka Hazina wa Kitaifa wa ODM Timothy Bosire, ambaye anatoka Nyamira, alitaja ghasia hizo kuwa mbinu za kisiasa zilizopitwa na wakati akizua maswali kuhusu mbona msafara huo ulishambuliwa Keumbu ilhali ulikuwa umepita maeneo mbalimbali kwa amani.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Sun, 05 Jul 2026 22:55:44
Aladwa awarai wanachama wa ODM wasusie maandamano Saba Saba
BAADHI ya viongozi wa ODM katika Kaunti ya Nairobi wamewataka wafuasi wao wasishiriki maandamano ya Saba Saba ambayo yanapangwa kufanyika hapo kesho. Wakiongea Nairobi Jumapili, viongozi hao walisema wao ni sehemu ya Serikali Jumuishi na njia ya kusaka suluhu kwa changamoto za nchi ni kupitia mazungumzo badala ya maandamano. Mbunge wa Makadara, George Aladwa, ambaye pia ni Mwenyekiti wa ODM Kaunti ya Nairobi alitoa wito wa umoja kati ya viongozi na akawataka polisi wahakikishe kuwa waandamanaji hawaharibu mali. "Tunasema hakuna mwanachama wetu ambaye atatumika kuzua ghasia jijini na taifa lote. Sote tuko katika Serikali Jumuishi na tunasema kuwa hatutaingia barabarani kwa ajili ya maandamano ya Saba Saba," akasema Bw Aladwa. Kauli yake ilijiri wakati ambapo wanaharakati wa kibinadamu wametoa wito wa kuandaliwa kwa maandamano kupinga kutoweka kwa watu kwa njia tatanishi na pia mauaji ya kiholela mikononi mwa polisi. Mbunge huyo aliwataka Waziri wa Usalama wa Ndani, Kipchumba Murkomen na Katibu wa wizara hiyo, Dkt Raymond Omollo kuwalinda Wakenya dhidi ya maandamano yoyote ambayo yanatishia amani ya nchi. Aidha waliwaonya wale ambao wamekuwa wakimshutumu Dkt Omollo kutokana na utendakazi wake, akisema katibu huyo ataendelea kuhudumu serikalini hadi 2027. "Katibu Omollo anafaa aruhusiwe kuendelea na kazi yake bila kuingiliwa. Wale ambao wana malalamishi dhidi yake wayafikishe katika afisi yake jumba la Harambee," akasema. Vilevile Bw Aladwa na viongozi alioandamana nao walisema Kenya ni nchi ambako uhuru wa vyombo vya habari unaheshimiwa katika kutia mizani utendakazi wa upinzani na serikalini. "Ni vyema iwapo vyombo vya habari vitamakinikia amani hata vikishutumu viongozi wa kisiasa. Kama utendakazi wangu ni duni, chombo cha habari kina uhuru wa kunimulika. Tunahitaji amani kuelekea uchaguzi wa 2027," akasema. Kuhusu uongozi wa ODM alipuuza mrengo wa Katibu Mkuu wa ODM Edwin Sifuna akisema wanaunga mkono ule wa Dkt Oburu Oginga.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Sun, 05 Jul 2026 23:55:46
2027: Mudavadi kimya watu wakijipanga
KIMYA na kukosekana kwa Kinara wa Mawaziri Musalia Mudavad katika mjadala wa nani atakuwa mgombeaji mwenza wa Rais William Ruto mnamo 2027 kumeibua maswali kuhusu mikakati yake ya kisiasa. Miezi michache iliyopita, kumekuwa na wito kutoka kwa viongozi mbalimbali kuhusu wale ambao wanastahili kuwa mgombeaji mwenza wa Rais Ruto 2027. Ndani ya Serikali Jumuishi, wanasiasa kutoka Mlima Kenya wamekuwa wakishinikiza wadhifa wa mgombeaji mwenza usalie kwa Naibu Rais Profesa Kithure Kindiki. Baadhi ya viongozi wa Magharibi mwa Nchi nao wanampigia upato Spika wa Bunge la Kitaifa, Moses Wetangula kwa wadhifa huo. Ndani ya ODM kuna kambi mbili ambazo zimezuka ambapo baadhi ya wanasiasa kutoka Pwani wanampigia upato Waziri wa Madini, Hassan Joho. Kwa upande mwingine wanasiasa kutoka Magharibi mwa Nchi nao wanamtaka Waziri wa Vyama vya Ushirika, Wycliffe Oparanya. Ndani ya upinzani, Kiongozi wa Linda Mwananchi, Edwin Sifuna ambaye anatoka Magharibi kama tu Bw Mudavadi, ameshabikiwa awe mgombeaji mwenza au hata mwaniaji wa urais. Mjadala kuhusu mgombeaji mwenza wa Rais Ruto ukishika, hakuna mwanasiasa anayeonekana kumakinikia Bw Mudavadi na haijulikani iwapo bado anataka kuwa rais baada ya uchaguzi mkuu wa 2027. Waziri huyo wa Masuala ya Kigeni amekuwa akimakinikia ziara ya Rais nje ya nchi akionekana kutomakinikia siasa za nchi. Mnamo Juni 13, akiwa ameandamana na Rais Ruto katika hafla ya kisiasa katika Chuo Kikuu cha Masinde Muliro, aliwaonya wakazi wa Magharibi dhidi ya kuingia mtego wa upinzani. "Kuna watu ambao wanajifanya wanatoa mwelekeo kwa jamii yetu ilhali walibanduliwa madarakani na hawajui hatima yao. Kama viongozi wenu tumeamua kuunga mkono kuchaguliwa tena kwa Rais Ruto,," akasema Bw Mudavadi. "Nilikuambia mnamo 2022 kuwa yeye ndiye njia na sasa bado ndiye njia. Lazima tusalie tumemakinika na watu wetu wasidanganywe," akongeza Bw Mudavadi. Waziri huyo, Bw Wetangúla na Bw Oparanya wanachukuliwa kama viongozi wakongwe kutoka Magharibi ambao wametawala siasa za eneo hilo kwa miaka mingi. "Shida ya Wetangúla na Mudavadi ni kwamba wanafikiria umri wao hausongi na ule wa Rais Ruto unasonga. Wetangula atakuwa na miaka 75 mnamo 2032 naye Mudavadi 71. Mbona wahisi watapewa urais na tunastahili kuwasubiri? Kama wangekuwa makini wao ndio wangekuwa wakimpa Rais Ruto mamlaka," akasema Bw Natembeya. Seneta wa Kakamega, Boni Khalwale naye anasema wakati huu watu wa Magharibi hawako na Bw Mudavadi na Wetangúla. "Sitaki nizungumze nionekane nawadharau ila ukweli ni kwamba mara hii watu hawako nao," akasema Seneta huyo. Seneta wa zamani wa Kakamega, Cleophas Malala ambaye ni naibu kiongozi wa DCP pamoja na wabunge Raphael Wanjala (Budalangí) na Junnet Mohamed (Suna Mashariki) pia wanampigia upato Bw Oparanya. Kwa upande mwingine Gavana wa Kakamega, Fernandes Baraza naye amemtaja Bw Wetangúla kama kigogo wa siasa wanayemuunga mkono kurithi nafasi ya Rais Ruto na hata anatosha kuwa mgombeaji mwenza. "Amekuwa nje ya nchi kwa mikutano na Rais Ruto na nahisi anaweza kuteuliwa mgombeaji mwenza wake. Wetangúla anaonekana kifua mbele kuliko Mudavadi kwa sababu amekuwa nyanjani na bado ana chama chake cha Ford Kenya," akasema Profesa Masibo Lumala, msomi na mchanganuzi wa masuala ya kisiasa.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Mon, 06 Jul 2026 00:55:00
2027: Mkutano wa faragha kati ya Gachagua, Wanjigi wazua gumzo
MKUTANO wa faragha kati ya aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua na Kiongozi wa Safina Jimi Wanjigi nyumbani kwake Wamunyoro kunaonekana kuvuruga hesabu za urais ndani ya muungano wa upinzani. Kumekuwa na madai kwa tikiti ya urais upinzani ni kati ya Kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka na mwenzake wa Jubilee Dkt Fred Matiangi huku Kiongozi wa Linda Mwananchi Edwin Sifuna akitathminiwa kuwa mgombeaji mwenza wa mmoja kati ya wanasiasa hao. Hata hivyo, kumekuwa na dhana kwamba iwapo hakutakuwa na kigogo wa siasa kutoka Mlima Kenya katika nafasi za juu huenda wapigakura wakakosa kujitokeza debeni. Bw Wanjigi ametangaza kuwa anasaka urais na kutokana na mfuko wake mzito baadhi ya vinara na wandani wao wameanza kuingiwa na wasiwasi hasa wale wanaoegemea mrengo wa Bw Musyoka.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Mon, 06 Jul 2026 01:55:52
Wakenya waliotimuliwa Afrika Kusini wazungumzia masaibu yao
BAADHI ya Wakenya wamesimulia kwa uchungu jinsi ambavyo walilazimika kurejea nchini kutoka Afrika Kusini ambako wenyeji wanawafurusha wageni. Juni 30 ilikuwa makataa ambayo raia wa Afrika Kusini walitoa kwa wahamiaji haramu kuondoka nchini humo wakiwakashifu kwa kunyakua nafasi za ajira pamoja na kutumia rasilimali zao. Ingawa Wakenya hawajalengwa sana, wiki jana serikali ilianza kuwarejesha nchini wale ambao wanatilia shaka usalama wao. Anthony Waweru ambaye amekuwa Afrika Kusini tangu 2022 akiwa dereva wa basi alisimulia jinsi ambavyo nyumba yake ilichomwa. Alisema alisikia kundi la watu likikaribia kwake usiku likiimba kwamba raia wa kigeni lazima waondoke bila mali yoyote. "Nilitoka mahala hapo wiki mbili zilizopita na kuenda kwingine kujificha," akasema. Bw Waweru alikuwa kati ya Wakenya 55 ambao walitua uwanja wa JKIA Alhamisi iliyopita saa 11 asubuhi. Alinufaikia mpango wa serikali wa kuwarejesha Wakenya wanaoishi nchini humo ambao usalama wao upo hatarini. Kufikia Jumamosi, serikali ilikuwa imewarejesha Wakenya 266 nchini kupitia mpango huo ambao Wizara ya Masuala ya Kigeni imesema utafikia tamati mnamo Alhamisi hii. "Wakenya ambao wanataka kurejeshwa nchini wanastahili kujisajili na ubalozi wa Kenya Afrika Kusini jijini Pretoria kufikia Alhamisi," ikasema wizara hiyo kupitia taarifa mnamo Ijumaa jioni. Bi Ruth Wambui, mfanyabiashara naye alirejea na watoto wake wawili akisema alikuwa kati ya wale ambao walitishiwa na hakuwa na budi ila kurejea nchini. "Mwanzoni nilikuwa sijaamua kurudi lakini baada ya kuona hasara na mali ambayo nimepoteza, nimeona ni afadhali nirejee nchini," akasema. Alifichua kuwa nyumba yake iliteketezwa mwaka jana katika njia tatanishi na pia biashara yake ilikuwa ikilengwa.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Mon, 06 Jul 2026 02:55:55
Mahakama yatoa uamuzi wa kihistoria kuhusu mzozo wa ardhi jijini Nairobi
RAMANI ya eneo iliyochorwa katika miaka ya 1980 ilitelekezwa kwa zaidi ya miongo mitatu kabla ya kujitokeza kuwa moja kati ya sakata kubwa zaidi kuhusu ardhi nchini. Kilichoanza kama mradi maalum wa makazi ya kibinafsi katika eneo la Kaskazini mwa Nairobi, kiligeuka kesi ya kulipwa fidia ya ShSh3.2 bilioni iliyovutia tume za kikatiba, wapelelezi wa kupiga vita ufisadi na korti, huku maafisa waking'ang'ana kujibu swali moja: Ni nani hasa alimiliki ardhi iliyojengwa shule mbili za umma? Wengine waliovutwa kwenye kashfa hiyo ni aliyekuwa waziri wa elimu, Fred Matiang'i baada ya wizara yake kukubali ushauri kutoka kwa Tume ya Ardhi Nchini (NLC) na kulipa awamu ya Sh1.5 bilioni ili kumiliki ardhi hiyo, ikibakisha salio la Sh1.7 bilioni. Kiini cha mzozo huo ni ekari 13.7 zilizojengwa Shule ya Msingi ya Drive-In na Shule ya upili ya Ruaraka High. Mzozo huo ulianza Disemba 1981 katika enzi ya Tume ya Jiji la Nairobi, jiji kuu lilipokuwa likipanuka kwa kasi huku wastawishaji wakifungua maeneo mapya ya ustawishaji. Kampuni za Afrison Export Import Limited na Huelands Limited zilinunua ardhi iliyosajiliwa kama LR No. 7879/4, yenye ekari 96 kutoka kwa kampuni kwa jina Joreth Limited. Ilichukua vilevile mkopo wa Sh21 milioni kutoka shirika la Continental Credit Finance Limited (lililofilisika) kufadhili ujenzi wa majumba 500 yenye ghorofa moja ya Kampuni ya Posta na Mawasiliano (KPTC). Rekodi za korti zilionyesha ustawishaji huo ulipangiwa kujumuisha takriban nyumba 1,200 ikiwemo barabara, mifereji ya majitaka, duka, vituo vya kijamii na ardhi iliyohifadhiwa kwa taasisi za umma, ikiwemo shule ya msingi na ya sekondari. Francis Mburu, mkurugenzi wa Afrison Export Import Ltd na Huelands Ltd, alieleza korti kampuni ilikataa masharti ya mpangilio kwa sababu, kwa maneno yake, "yalikuwa makali na yasiyoweza kutimizwa kifedha." Mvutano huo uliingia awamu mpya 2015 wakati Bw Mburu aliwasilisha kesi ya kihistoria kuhusu ukiukaji wa haki kuhusu ardhi kwa NLC. Korti ya rufaa iliunga mkono uamuzu kuwa ardhi ya shule ilijumuisha sehemu ya ardhi iliyotengewa shughuli za umma na kukataa jaribio la wastawishaji kubatilisha uamuzi wa korti ya Mazingira na Ardhi. Uamuzi huo pia ulizima ombi lao la kudai Sh1.76 bilioni walizohoji zilisalia baada ya malipo ya kwanza ya Sh1.5 bilioni. "Tumebaini kuwa shule hizo zipo kwenye ardhi ya umma kwani NlC haikuwa na msingi kisheria wa kuitwaa kwa lazima, walisema majaji wa korti ya Walibaini kuwa mpango wa makazi uliidhinishwa na walalamishi wakawezesha ujenzi wa nyumba 196 za GSU kuambatana na mradi ulioidhinishwa. "Ushahidi uliorekodiwa vilevile unathibitisha usalimishaji bayana. Barua ya Julai 4, 1984 kutoka kwa wakala wa walalamishi kinathibitisha hali ya kuafikiana kuhusu usalimishaji huu," walisema majaji.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Mon, 06 Jul 2026 06:34:53
Walimu watoa notisi ya kugoma kusimamia mitihani mwaka huu
WALIMU waliokuwa wasimamizi, wasahihishaji na waangalizi wa mitihani ya kitaifa mwaka jana wameonya kuwa huenda wakasusia shughuli za mitihani ya mwaka huu ikiwa serikali haitawalipa marupurupu yao ambayo yamecheleweshwa kwa zaidi ya miezi minane. Hatua hiyo inatishia maandalizi ya mitihani ya kitaifa ya 2026 huku vyama vya walimu vikisema vitawashauri wanachama wao kutohudhuria mafunzo ya Baraza la Mitihani la Kenya (KNEC) wala kusimamia na kusahihisha mitihani hadi watakapolipwa. Katika hotuba ya bajeti ya mwaka wa kifedha 2026/2027 iliyosomwa Juni 11, Waziri wa Fedha John Mbadi aliwahakikishia wabunge kuwa Sh1.5 bilioni zinazodaiwa na walimu wanaosimamia mitihani zingelipwa kabla ya Juni 30, mwisho wa mwaka wa fedha 2025/2026. Hata hivyo, tarehe hiyo ilipita bila walimu kulipwa. Afisa mmoja wa KNEC alisema baraza hilo haliwezi kulipa fedha ambazo halilipwa na Wizara ya Fedha. Kucheleweshwa kwa malipo hayo kumeathiri maelfu ya walimu waliosimamia mtihani wa KCSE, Tathmini ya Elimu ya Msingi (KPSEA) na Tathmini ya Shule za Sekondari za Awali (KJSEA) mwaka 2025. Kulingana na stakabadhi za bajeti, KNEC ilihitaji Sh12.7 bilioni kuendesha mitihani hiyo lakini ilitengewa Sh5.9 bilioni pekee katika bajeti ya awali. Zaidi ya Sh1 bilioni zilitumika kulipa madeni ya mwaka uliotangulia, hali iliyoacha pengo kubwa la fedha. Ingawa baadaye wizara ilitoa Sh3.1 bilioni kupitia bajeti ya ziada bado kulisalia upungufu wa takriban Sh4.76 bilioni.Walimu wanasema ahadi za serikali hazijawasaidia. Ogoro Miruka wa Shule ya Msingi ya Lang'ata West alisema alisimamia mitihani kwa siku 12 kwa malipo ya Sh500 kwa siku lakini hajapokea hata senti moja. "Hadi sasa hatujalipwa licha ya ahadi nyingi kutoka serikalini. Walimu wanapaswa kufikiria kususia mitihani ya mwaka huu," alisema. Mwalimu mwingine ambaye hakutaka kutajwa jina alisema kucheleweshwa kwa malipo kumevunja moyo walimu wengi. "Hapo awali tulilipwa mara tu matokeo yalipotangazwa, lakini wakati huu hakuna aliyelipwa licha ya ahadi za mara kwa mara," alisema. Evans Ochieng' wa Shule ya Riruta Satellite Junior alisema hata baadhi ya wasahihishaji wa mitihani bado hawajalipwa kikamilifu. Naibu Katibu Mkuu wa KUPPET, Moses Nthurima, alisema kucheleweshwa kwa malipo kwa miezi minane hakukubaliki. "Serikali inapaswa kuhakikisha shughuli muhimu kama hizi zinafadhiliwa kwa wakati, la sivyo ubora wa elimu utaathirika," alisema. Katibu Mtendaji wa KNUT tawi la Nairobi, Mugwe Macharia, alisema walimu wamekuwa wakipiga simu ofisi za chama wakitaka hatua ichukuliwe. "Ikiwa fedha hazitalipwa, tutawashauri wanachama wetu wasihudhurie mafunzo ya KNEC na tunazingatia pia kuwashauri wasisimamie mitihani ya mwaka huu," alisema.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Mon, 06 Jul 2026 07:48:34
MAONI: Kalonzo ajitafutie kura la sivyo atarukwa kama 2013
KINARA Wiper Kalonzo Musyoka anastahili kutafuta kura zake kwanza kabla ya kutegemea uungwaji mkono wa viongozi wenzake kwa sababu suala la kuidhinishwa kwake huenda likagawanya upinzani kuelekea uchaguzi mkuu wa 2027. Wiki jana kulikuwa na gumzo kuhusu kauli ya aliyekuwa Naibu wa Rais Rigathi Gachagua kuwa hana muafaka wowote wa kuunga azma ya makamu huyo wa rais wa zamani. Bw Gachagua ambaye amekuwa na kikao cha kuwasikiliza wanasiasa na makundi mbalimbali ya kijamii nyumbani kwake Wamunyoro, Nyeri, aliweka bayana kuwa hakuna maafikiano yoyote kati yake na Bw Musyoka kuhusu 2027 na kuwa mazungumzo bado yanaendelea. Katika ziara aliyokuwa nayo Ukambani mnamo Machi 30 2026, Bw Gachagua alimmiminia Bw Musyoka sifa kedekede na kuashiria kuwa atakuwa nyapara wa upinzani katika kinyang'anyiro cha urais mwakani. Katika msururu wa mikutano ya siku tano Ukambani, Bw Gachagua alimrejelea Kalonzo kama msemaji wa upinzani huku pia akisema ana uzoefu wa uongozi kumwezesha kuwa rais wa sita wa Kenya. Zaidi ya miezi mitatu baadaye, mambo yanaonekana kubadilika huku Bw Gachagua akibadili wimbo na kauli zake nyingi zikimnukuu akisema yuko tayari kuunga mtu yeyote katika upinzani lakini baada ya mazungumzo. Wandani wa Bw Musyoka kama vile Seneta wa Kitui, Enock Wambua nao wamekuwa wakirindima ngoma ya Bw Musyoka na kusisitiza kuwa ataungwa mkono na Mlima Kenya. Hata hivyo, Bw Musyoka anastahili kujihadhari na kuanza kujitafutia kura badala ya kutegemea tu za Mlima Kenya. Kuelekea uchaguzi mkuu wa 2013, Bw Musyoka alikuwa mshirika wa Uhuru Kenyatta na William Ruto na wakati wa mazungumzo ya kusaka muafaka wa uchaguzi, alipigwa kumbo kutokana na kura zake zilizoonekana kuwa chache. Hii ndiyo hali itakayomkabili tena kwa sababu Bw Gachagua mwenyewe amewahi kumshajiisha aje mezani na kura nyingi. Ni dharau ya kutokuwa na kura nyingi 2013 ndiyo iliyosababisha aondoke kambi ya UhuRuto na kuwa mgombeaji mwenza wa Raila Odinga. Kwa muda sasa Bw Musyoka amekita siasa zake Ukambani na wakati mwingine Mlima Kenya. Amekuwa akienda ziara maeneo mengine tu iwapo vinara wa upinzani wanahudhuria mikutano maeneo hayo. Makamu huyu wa rais wa zamani anafaa kuzinduka na aanze kujitafutia kura Nyanza, Pwani, Magharibi, Bonde la Ufa na Kaskazini Mashariki badala ya kutegemea Mlima Kenya pekee. Akumbuke kuwa mbali na DCP, Naibu Kiongozi wa Jubilee Dkt Fred Matiang'i pia analenga kura za eneo hilo 2027. Kwa hivyo, Bw Musyoka hajahakikishiwa uungwaji kutoka Mlima Kenya kiasi cha kufananishwa na walivyompigia Rais Ruto 2022 au Uhuru na Kibaki kwenye chaguzi za nyuma. Eneo la Ukambani lina Kaunti za Machakos, Kitui na Makueni kulingana na makadirio ya Tume ya Uchaguzi (IEBC) mnamo 2027, Machakos itakuwa na wapigakura 883, 629, Kitui kura 684,878 kisha Makueni 616,104 kufikia 2027. Hizi ni karibu kura milioni mbili ambazo hazitoshi kumpa Bw Musyoka urais ndiposa lazima asake uungwaji mkono kwa maeneo yote badala ya mlima pekee ambayo pia hana uhakika nao. Isitoshe wakazi wa Mlima Kenya nao wanaangalia watashikilia wadhifa upi wa juu na kauli ya kila mara ya Bw Gachagua kuwa atawania urais inastahili kumtia Bw Musyoka wasiwasi. Ni wazi suala la Kalonzo kuwa mwaniaji wa upinzani limeibua wasiwasi na mgawanyiko miongoni mwa vinara wa upinzani. Faraja kwake itakuwa ni kuzidisha juhudi kuwahi kura nyingi la sivyo atarukwa kama 2013. Siasa haina urafiki wa milele na hakikisho la kudumu.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Mon, 06 Jul 2026 08:40:57
Iran waapa watalipiza kisasi dhidi ya Amerika na Israel kwa kifo cha Ayatollah
TEHRAN, Iran: RAIA wa Iran Jumatatu, Julai 6, 2026 waliapa kuwa lazima nchi hiyo ilipize kisasi cha mauaji ya Kiongozi wa Kidini Ayatollah Ali Khamenei wakielekeza hasira zao kwa Amerika na Israel. Khamenei aliuawa mnamo Februari 28, siku ya kwanza ya Amerika na Israel kutekeleza mashambulizi dhidi ya Iran. Maelfu ya raia wa Iran walijitokeza katika msafara wa mazishi ya Khamenei yaliyofanyika viungani mwa jiji la Tehran. Msafara huo ulikuwa wa kumuaga rasmi kiongozi huyo wa kidini. Jumatatu ilikuwa siku kubwa zaidi katika wiki yenye shughuli nyingi za maombolezo. Picha za angani zilizorushwa na televisheni ya taifa zilionyesha maelfu ya waombolezaji wakiwa wamefurika katika barabara kuu katikati mwa mji wa Tehran. Majeneza ya kiongozi huyo aliyeuawa pamoja na jamaa wanne wa familia yake yalipelekwa, kupitia mitaa ya jiji hilo, kwa kutumia lori kubwa, huku magari ya wazimamoto yakinyunyiza maji kutoka juu ili kupunguza joto kwa waombolezaji. Msafara huo ulipopita chini ya daraja, waombolezaji walirusha mawe kuelekea bango lililokuwa limetundikwa juu likimwonyesha Rais wa Amerika Donald Trump akiwa amelengwa kwa risasi kichwani. "Amerika ilimuua baba yetu. Hatutawaacha mponyoke", likasema maneno kwenye bango hilo. Waombolezaji walikuwa wakipeperusha bendera za Iran pamoja na mabango mekundu. Mabango hayo yaliandikwa "walipiza kisasi wa Khamenei," ikiwa ni kauli yenye umuhimu mkubwa katika Uislamu wa Kishia tangu mjukuu wa Mtume Muhammad alipouawa vitani katika karne ya saba. Mnamo Jumapili, wana watatu wa kiongozi huyo aliyeuawa waliomba kando ya jeneza lake katika ukumbi mkubwa wa sala mjini Tehran. Hata hivyo, Mojtaba Khamenei, ambaye alimrithi baba yake kama Kiongozi Mkuu wa Iran, hakujitokeza hadharani. Inaaminika kuwa alipata majeraha yaliyomsababishia ulemavu wa uso katika shambulizi lililomuua baba yake. Tangu vita vilipoanza Februari 28 kufuatia mashambulizi ya anga ya Israel na Amerika dhidi ya Iran, Mojtaba hajaonekana tena hadharani. Shughuli za maombolezo zilianza Ijumaa wakati majeneza ya Khamenei mkubwa, mmoja wa mabinti zake na mtoto wake mwenye umri wa miezi 14, mmoja wa wakwe zake, pamoja na mke wa Mojtaba yalipowekwa kwa ajili ya viongozi wa Iran na wageni wa heshima kutoka mataifa mbalimbali kutoa heshima zao za mwisho. Sherehe nyingine kubwa za maombolezo zilifanyika nje siku za Jumamosi na Jumapili kabla ya msafara mkubwa wa mazishi ya Jumatatu. Baadaye wiki hii, mwili wake utapelekwa katika misafara mingine ya mazishi katika mji wa Qom, ambao ni kitovu cha mafunzo ya Kishia n Iran, na pia katika miji miwili ya Iraq yenye maeneo matakatifu ya Kishia. Baada ya hapo utarejeshwa Iran kwa ajili ya mazishi katika eneo la kihistoria la makaburi ya Mashhad. Vita hivyo vilimalizika baada ya makubaliano ya awali ya amani yaliyofikiwa mwezi uliopita. Viliwaacha viongozi wa kidini wa Iran wakiendelea kubaki madarakani huku wakitangaza ushindi, na kudai kuwa wameongeza ushawishi wao kupitia udhibiti wa njia ya usafirishaji wa mafuta wa Strait of Hormuz. Trump pia amedai ushindi, ingawa malengo aliyoyataja mwanzoni mwa vita ya kuharibu uwezo wa Iran wa nyuklia na makombora, kuzuia uwezo wake wa kushambulia nchi jirani, na kuweka mazingira yatakayowawezesha raia wa Iran kuwaondoa viongozi wao madarakani, hayajatimia. Trump alisema mwishoni mwa wiki kwamba mazungumzo ya amani kati ya Amerika na Iran yameahirishwa kwa wiki moja kutokana na shughuli za mazishi. Waziri wa Ulinzi wa Israel, Israel Katz, alisema Jumatatu kuwa Khamenei mkubwa aliuawa kwa sababu aliongoza mpango wa kuiangamiza Israel. "Kiongozi yeyote wa Iran atakayejaribu tena kutekeleza mipango ya kuiangamiza Israel atauawa pia," akasema Katz.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Mon, 06 Jul 2026 10:45:56
Nairobi Police boss declares Tuesday a working day, warns Saba Saba gatherings will be illegal
Nairobi Regional Police Commander Issa Mohamud has declared Tuesday, July 7, a normal working day, saying no formal notification has been received for any planned protests in the city and warning that any gathering held without notification will be treated as illegal. Observed annually on July 7, Saba Saba commemorates the 1990 movement that pushed [...] The post Nairobi Police boss declares Tuesday a working day, warns Saba Saba gatherings will be illegal appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Mon, 06 Jul 2026 10:23:39
At least 25 killed in Sri Lanka prison riots
At least 25 people have been killed four of them guards and more than 100 injured in prison riots in western Sri Lanka. The two days of violence at Negombo Prison, in a coastal town north of Colombo, began with clashes between two groups of inmates. Prisoners are alleged to have grabbed prison [...] The post At least 25 killed in Sri Lanka prison riots appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Mon, 06 Jul 2026 10:32:48
Buckingham Palace says Prince Harry will not stay at palace
Buckingham Palace says Prince Harry will not be staying at the palace during his visit to London this week, despite his team announcing this morning that he had accepted an invitation to do so. Royal sources said the duke had not responded in time to the offer of accommodation at a royal residence and that [...] The post Buckingham Palace says Prince Harry will not stay at palace appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Mon, 06 Jul 2026 10:39:00
Court orders closure of case against woman accused of tracking Ruto's flights
Mombasa based social media influencer Halima Ngachia, popularly known as Princess Halima, appeared before the magistrates court on Monday morning, where investigators sought more time to examine electronic gadgets seized from her. After considering the submissions, the court ordered that the miscellaneous application be closed. Halima is accused of operating an X account that allegedly [...] The post Court orders closure of case against woman accused of tracking Ruto's flights appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Mon, 06 Jul 2026 09:42:30
UK fighter jets intercept Russian plane over Norwegian Sea
UK fighter jets intercepted a Russian maritime patrol aircraft after it repeatedly approached a carrier strike group in the Norwegian Sea, the Ministry of Defence (MoD) said. The Russian Bear-F plane passed at low altitude and unnecessarily close to the HMS Prince of Wales aircraft carrier and is believed to have dropped 10 sonobuoys into [...] The post UK fighter jets intercept Russian plane over Norwegian Sea appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Mon, 06 Jul 2026 09:52:57
Hamas has dissolved its governing body in Gaza, ending 20 years of rule there
In a move that marks the most significant political shift in Gaza in nearly two decades, Hamas announced today the dissolution of its de facto government, clearing the way for a U.S.-backed technocratic committee to assume civilian administration of the Palestinian territory. The announcement, made at a press conference in Deir al-Balah, central Gaza, comes [...] The post Hamas has dissolved its governing body in Gaza, ending 20 years of rule there appeared first on Kahawatungu.
read moreRight Column Content