taifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Mon, 13 Jul 2026 00:55:17
Vita vya mamlaka Senegal korti ikizima Sonko kumvua Faye madaraka kupitia bunge
DAKAR, Senegal: MAHAKAMA ya Juu ya Senegal imeondoa marekebisho kwenye katiba ya taifa hilo ambayo yangebadilisha usawazishaji wa mamlaka serikalini. Korti ilibaini kuwa marekebisho hayo yaliyopitishwa na kuidhinishwa na Bunge la Kitaifa mnamo Juni 29, yalienda kinyume na katiba. Kati ya marekebisho hayo yalikuwa yale ya kumzuia rais aliye madarakani kuhudumu kama kiongozi wa chama cha kisiasa. Rais wa Senegal Bassirou Diomaye Faye wiki jana alisema alikuwa anapanga kuanzisha chama chake cha kisiasa. Shinikizo za kubadilisha katiba zimekuwa zikiendeshwa na chama tawala cha Pastef ambacho kinaongozwa na Spika na aliyekuwa Waziri Mkuu Ousmane Sonko. Wakosoaji wanasema marekebisho hayo yalikuwa njama ya mrengo wa Sonko kutwaa mamlaka. Faye alimtimua Sonko kama mkuu wa serikali mnamo Mei. Mahakama hiyo ya kikatiba ilisema Faye aliiomba iangazie marekebisho hayo na ibaini iwapo wanasiasa wa upinzani walikuwa wamefuata sheria. Uhasama kati ya Sonko na Faye ambao walikuwa washirika wa zamani, huenda ukakwamisha juhudi za Senegal za kupata suluhu kuhusu malipo ya madeni mengi ambayo yameisakama. Sonko alisema anaheshimu uamuzi wa mahakama.
read morekenyanews.go.ke
@kna Mon, 13 Jul 2026 09:14:01
ODM to back President William Ruto's re-election bid
ODM will not field a presidential candidate in the next years General Election and will instead back President Rutos re-election bid, Party leader Oburu Oginga has declared. Oburu made the revelation during a fundraiser at Chiga Catholic Church in Homa Bay Town Constituency noting that negotiations for pre-election agreement with the Presidents team was now...
read morekenyanews.go.ke
@kna Mon, 13 Jul 2026 09:16:43
Maintain stringent biosafety protocols in confined field trials, urges NBA
Kenya's National Biosafety Authority (NBA), which is mandated to regulate research activities involving genetically modified organisms (GMOs), has urged research institutions conducting Confined Field Trials (CFTs) to strictly comply with the biosafety protocols stipulated in the Biosafety Act, 2009. Speaking during a visit to the Kenya Agricultural and Livestock Research Organization (KALRO) research facilities at Muguga (Biotechnology Research...
read morekenyanews.go.ke
@kna Mon, 13 Jul 2026 09:20:37
AKEFEMA calls for strategic investment in quality animal feed production
The Association of Kenya Feed Manufacturers (AKEFEMA) has called for increased investment in quality animal feed production, saying it is critical to boosting livestock productivity, strengthening food security, and transforming Kenya's agricultural sector. Speaking ahead of the AKEFEMA Feeds Exhibition and Conference (AFEC) 2026, AKEFEMA Chairman Joseph Karuri said the livestock industry must become more...
read morekenyanews.go.ke
@kna Mon, 13 Jul 2026 09:22:44
Modern beekeeping 'sweetens' farmers' incomes
For generations, maize farming has been the backbone of livelihoods in Lugari Sub-County, Kakamega County. But as climate change, declining soil fertility and rising production costs continue to erode profits, an increasing number of farmers are turning to modern beekeeping as a sustainable and lucrative alternative that is transforming household incomes while supporting environmental conservation....
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Mon, 13 Jul 2026 09:05:10
Bei ya mafuta yaanza kupanda tena baada ya Amerika kurejelea vita na Iran
TEHRAN, Iran: MASHAMBULIZI baina ya wanajeshi wa Amerika na Iran yaliyoendelea tokea wikendi yamechangia kupanda tena kwa bei ya mafuta ulimwenguni. Iran ililenga vituo vya kijeshi vya Amerika katika eneo la Ghuba na kutangaza kuwa imefunga tena Mlango-bahari wa Hormuz. Wanajeshi wa Iran Jumatatu walisema walilenga kambi za jeshi la Amerika nchini Bahrain na Kuwait na kuharibu vifaa vya kijeshi nchini Oman. Pia Iran ilishambulia ghala la silaha katika kambi ya jeshi la Anga la Prince Hassan nchini Jordan huku ikilipiza kisasi shambulizi lolote linalotekelezwa na Amerika. Amerika nayo ilishambulia mifumo ya ulinzi wa anga ya Iran, kambi ya jeshi pwani na boti za kijeshi. Ilitumia ndege za kivita, meli za kijeshi na ndege zisizo na rubani (droni). Mapigano hayo yanaonyesha kuwa muafaka wa kusitisha vita kati ya nchi hizo mbili sasa umekiukwa. Muafaka huo uliafikiwa mnamo Juni na ulilenga kufungua Mlango-bahari wa Hormuz na kusitisha vita kabisa kwa siku 60. Katika mahojiano mafupi na Reuters Jumapili, Rais wa Amerika Donald Trump alitabiri kuwa mara hii watalemea Iran katika vita hivyo. "Tunawashinda vibaya," akasema Trump. Kiongozi huyo tayari ameweka wazi kuwa hatilii manani muafaka uliotiwa saini ambao anasema umekufa japo akasema iwapo Iran inataka kunusurika bado kutakuwa na mazungumzo. Mwakilishi wa Iran kwenye mazungumzo na Amerika, Mohammad Baqer Qalibaf amesema kuwa wapo tayari kwa vita na hawatakubali kuhadaiwa tena. "Enzi za makubaliano yanayoegemea upande mmoja zimekwisha. Tuliwaambia watimize ahadi zeo au walipe gharama na sasa ukweli unaonekana," akasema. Vita vilivyoanzishwa na Amerika-Israel dhidi ya Iran mnamo Februari 28 vimevuruga usalama katika eneo la Ghuba na kuenea katika Mashariki ya Kati. Iran imeonyesha uwezo mkubwa wa kijeshi na umekuwa ukishambulia kambi za wanajeshi wa Amerika Mashariki ya Kati. Vita hivyo vimesababisha maelfu ya watu kuuawa, wengi wao wakiwa Iran na Lebanon. Iran imezima shughuli katika Strait of Hormuz na sasa kando na bei ya mafuta kupanda kuna mfumuko wa bei ya bidhaa kote ulimwenguni. Aidha Iran inasisitiza kuwa itafungua mkondo huo na kuruhusu meli za kupitisha mafuta iwapo Amerika itazima shughuli za kijeshi katika Pwani yake.
read morekenyanews.go.ke
@kna Mon, 13 Jul 2026 08:52:39
Kiambu PWD's receive food hampers
The Kiambu County Government has distributed food hampers to 120 persons with disabilities in Gitothua Ward, reaffirming its commitment to strengthening social protection programs for vulnerable residents across the county. The exercise, spearheaded by the Directorate of Gender and Social Services under the Department of Education, Gender, Culture and Social Services, forms part of the...
read morekenyanews.go.ke
@kna Mon, 13 Jul 2026 08:57:21
County creates corporation to strengthen agricultural services
Bungoma Governor Kenneth Lusaka has signed into law the Bungoma County Agriculture Institutions Development Corporation Act, 2025, paving the way for the establishment of a Sh230 million corporation to oversee, finance and modernize key agricultural institutions across the county. The new law creates the Bungoma County Agriculture Institutions Development Corporation, a body mandated to manage...
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Mon, 13 Jul 2026 08:39:52
Kampuni inavyotumia ubunifu kuvutia wateja wa maua
WAKATI mamia ya wageni wa humu nchini na kutoka mataifa mbalimbali walipofurika katika Maonyesho ya Kimataifa ya Kibiashara ya Maua (IFTEX) jijini Nairobi, kampuni moja ya Kenya ilivutia wengi kwa ubunifu wa kipekee uliosimamisha shughuli katika Ukumbi wa Visa Oshwal. Banda la Ole Engai Growers lilikuwa miongoni mwa yaliyopigwa picha zaidi katika maonyesho hayo ya mwaka huu, 2026 baada ya kuwasilisha sanamu ya farasi mwenye ukubwa wa wastani wa mnyama huyo, iliyotengenezwa kwa maua mabichi yaliyolimwa kwenye mashamba ya kampuni hiyo. Farasi huyo wa maua, aliyebuniwa kuadhimisha Mwaka wa Farasi katika kalenda ya Mwaka Mpya wa Kichina, aliunganisha sanaa na kilimo kwa njia iliyovutia wageni katika maonyesho yaliyofanyika kati ya Juni 2 na 4. Sanamu hiyo ilionekana kana kwamba ilikuwa hai kutokana na umbo lake lililoundwa kwa ustadi mkubwa, likiwa na kichwa, manyoya shingoni, mwili na miguu iliyopambwa kwa maua meupe, ya kijani na ya krimu. Ua aina ya gypsophila ndilo lililotumika zaidi kuunda mwili wa farasi huyo, likimpa mwonekano mweupe na laini kama wingu. Muundo huo uliashiria nguvu, kasi na ustahimilivu—sifa zinazohusishwa na farasi katika utamaduni wa Kichina, na pia ukuaji wa kampuni hiyo katika sekta ya maua. "Mwaka huu, 2026, ni Mwaka wa Farasi kulingana na kalenda ya Kichina. Tulitaka kuonyesha nguvu, ukuaji na uvumilivu kama kampuni kupitia maua tunayozalisha wenyewe," alisema Mkurugenzi Mwenza kampuni hiyo, Anjili Shah. Anjili alieleza kuwa wazo hilo lilibuniwa na timu ya kiufundi ya kampuni ikiongozwa na mbunifu mkuu ambaye amekuwa akiandaa mabanda yaliyoshinda tuzo katika maonyesho ya IFTEX kwa miaka kadhaa. Ubunifu huo uliiwezesha Ole Engai Growers kutwaa Tuzo ya Fedha ya Ubora wa Ubunifu (Silver Award for Design Excellence), baada ya mwaka uliopita kushinda tuzo ya banda bora zaidi. [caption id="attachment_190053" align="aligncenter" width="300"] Tuzo ya Ole Engai Growers baada ya kutumia muundo wa farasi wenye mvuto wakati wa Maonyesho ya IFTEX 2026. Picha|Sammy Waweru[/caption] Mwanzilishi mwenza na mkurugenzi wa kampuni hiyo, Sanir Shah, alisema maonyesho hayo yalionyesha uwezo wa kampuni hiyo kuzalisha maua ya kiwango cha juu na kubuni kazi za kipekee bila kutegemea maua kutoka kwa wazalishaji wengine. "Ole Engai Growers huzalisha maua katika shamba lenye ukubwa wa karibu hekta 29 eneo la Kaptagat, Eldoret, Kaunti ya Uasin Gishu," Sanir alifichua. Mbali na gypsophila, kampuni hiyo pia hulima maua aina ya delphinium ya rangi mbalimbali, asters, kangaroo paws, dianthus na kiwi mellow kulingana na mahitaji ya soko. Kulingana na Sanir, kampuni hiyo huuza nje takribani tani 1,200 za maua kila mwaka, masoko makubwa yakiwa Ulaya huku Mashariki ya Kati ikiandikisha ukuaji wa oda. Hata hivyo, alisema sekta hiyo inakabiliwa na changamoto kubwa kutokana na kupanda kwa gharama za usafirishaji wa mizigo kwa njia ya ndege. "Miaka mitano iliyopita tulikuwa tukilipa karibu Dola 1.4 za Amerika kwa kilo moja ya maua kusafirishwa. Sasa gharama imevuka Dola 4 kwa kilo. Hii imeathiri faida yetu," alisema. Baraza la Maua Kenya (KFC), pia, limeeleza kuwa gharama hizo zimeongezeka kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta, jambo linaloongeza gharama za usafirishaji wa bidhaa zinazoharibika haraka kama maua. [caption id="attachment_190054" align="aligncenter" width="300"] Ole Engai Growers huzalisha maua katika shamba lenye ukubwa wa karibu hekta 29 eneo la Kaptagat, Eldoret, Kaunti ya Uasin Gishu. Picha|Sammy Waweru[/caption] "Kwa sasa, usafirishaji pekee unachangia zaidi ya asilimia 40 ya gharama zote za kuuza maua nje wakati wa msimu wa mauzo bora," anasema Clement Tulezi, Afisa Mkuu Mtendaji KFC. Aidha, bei ya mbolea imeongezeka kwa karibu asilimia 25 huku gharama za uzalishaji zikiongezeka kwa kati ya asilimia 20 na 30. Changamoto nyingine ni mabadiliko ya tabianchi ambayo yamevuruga ratiba za uzalishaji kutokana na mvua zisizotabirika. Anjili alisema hali hiyo imefanya upangaji wa shughuli za shambani kuwa mgumu zaidi. Licha ya changamoto hizo, Ole Engai Growers inaendelea kupanua uzalishaji na kutafuta masoko mapya, hasa Mashariki ya Kati ya nchi za Uarabuni. Kwa ujumla, sekta ya maua nchini Kenya inaendelea kuwa mhimili muhimu wa uchumi. Mwaka 2025 iliiingizia nchi karibu Dola milioni 845 za Amerika (zaidi ya Sh110 bilioni), huku Kenya ikiendelea kuuza maua katika zaidi ya nchi 60 duniani, asilimia 70 ya mauzo hayo yakielekezwa katika soko la Umoja wa Ulaya (EU).
read morestandardmedia.co.ke
@standard Mon, 13 Jul 2026 08:39:03
Wetang'ula risks jail over alleged breach of court orders on political campaigns
The High Court has certified as urgent a contempt application seeking to have Speaker Moses Wetangula jailed for at least one month or fined Sh725,017 for each political engagement.
read morekenyanews.go.ke
@kna Mon, 13 Jul 2026 08:13:27
Road upgrade to stimulate economic growth
The completion of the upgrading of the Timboroa–Meteitei–Kopere Road is expected to usher in a new era of economic growth and improved connectivity for residents of Tinderet Sub County and neighbouring regions. The road, which links Nandi County to Uasin Gishu, has for years been a critical transport corridor for farmers, traders, transporters and travelers....
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Mon, 13 Jul 2026 07:55:55
Mike Maignan Siblings: All About Laura and Jessica
Mike Peterson Maignan is a professional footballer who plays as a goalkeeper and captains Serie A club AC Milan. Born on July 3, 1995, in Cayenne, French Guiana, he represents the France national team. Maignan is widely regarded as one of the top goalkeepers in world football, known for his shot-stopping abilities, distribution, and commanding [...] The post Mike Maignan Siblings: All About Laura and Jessica appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Mon, 13 Jul 2026 07:58:52
Samuele Ricci Siblings: Getting to Know Sara
Samuele Ricci is an Italian professional footballer born on August 21, 2001, in Pontedera, Italy. He plays as a midfielder, primarily as a deep-lying playmaker or box-to-box midfielder, and is currently at AC Milan in Serie A. Known for his technical ability, positional sense, and versatility, Ricci has been regarded as one of Italys promising [...] The post Samuele Ricci Siblings: Getting to Know Sara appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Mon, 13 Jul 2026 08:02:37
Pervis Estupiñán Siblings: A Look at the Footballer's Family Tree
Pervis Josué Estupiñán Tenorio is an Ecuadorian professional footballer who plays as a left-back and left wing-back for Serie A club AC Milan and the Ecuador national team. Born on January 21, 1998, in Esmeraldas, Ecuador, he is known for his attacking flair from the left flank, pace, crossing ability, and defensive solidity. Estupiñán has [...] The post Pervis Estupiñán Siblings: A Look at the Footballers Family Tree appeared first on Kahawatungu.
read morekenyanews.go.ke
@kna Mon, 13 Jul 2026 07:47:00
Champion early intervention for children with Neurodevelopmental disabilities
More than 300 teachers, caregivers, community health workers, and disability inclusion champions are undergoing a free four-month training programme aimed at improving early identification, support, and inclusion of children with neurodevelopmental disabilities. The training, organized by the Orione Community Training Centre in Kandisi in partnership with the Manos Unidas Foundation of Spain under the Inclusive...
read moreRight Column Content