kahawatungu.com
@kahawatungu Sat, 11 Jul 2026 02:19:48
Harambee Sacco loses bid to revive appeal in Nairobi land dispute
Harambee Sacco has suffered a legal setback after the Court of Appeal declined to extend the time for the Sacco to pursue an appeal in a long-running land dispute, leaving intact orders requiring it to transfer three Nairobi properties to Toshike Construction Company. In a ruling delivered on July 3, Court of Appeal Judge A.O. [...] The post Harambee Sacco loses bid to revive appeal in Nairobi land dispute appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Sat, 11 Jul 2026 02:33:02
DCI extradites Afghan national to US over alleged drug trafficking and firearms offences
The Directorate of Criminal Investigations (DCI), through its Anti-Narcotics Unit (ANU), has extradited an Afghan national wanted in the United States over alleged involvement in an international narcotics trafficking conspiracy and related firearms offences. In a statement, the DCI said Abdul Zahir Qadeer, also known as Haji Abdul Zahir, was extradited on July 9, 2026, [...] The post DCI extradites Afghan national to US over alleged drug trafficking and firearms offences appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Sat, 11 Jul 2026 01:48:24
How to Book Flights with Vitality
Vitality Travel allows eligible Discovery Bank and qualifying Vitality members to book local and international leisure flights while enjoying travel discounts, Discovery Miles payment options, and other travel benefits. Flight bookings can be made through the Discovery Bank app or the Vitality Travel platform on desktop. Learning how to book flights with Vitality can help [...] The post How to Book Flights with Vitality appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Sat, 11 Jul 2026 01:52:32
How to Book Movie Tickets Online
Booking movie tickets online is a fast and convenient way to reserve your seats before arriving at the cinema. Most cinemas allow customers to browse movie schedules, choose their preferred seats, and pay securely through a website or mobile app. Learning how to book movie tickets online can save you time, help you avoid long [...] The post How to Book Movie Tickets Online appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Sat, 11 Jul 2026 01:56:12
How to Borrow Data from MTN
MTN allows eligible prepaid customers to borrow data when they run out of their existing data balance. The borrowed data can help you stay connected for browsing, messaging, or other online activities, with the amount borrowed being deducted from your next recharge together with any applicable service fee. Learning how to borrow data from MTN [...] The post How to Borrow Data from MTN appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Sat, 11 Jul 2026 02:06:00
How to Borrow Money as a SASSA Grant Recipient
Many South Africans who receive grants from the South African Social Security Agency (SASSA) look for ways to access credit during financial emergencies. However, SASSA itself does not provide loans or lend money to grant beneficiaries. If you need to borrow money, you should only use registered and reputable financial institutions that comply with South [...] The post How to Borrow Money as a SASSA Grant Recipient appeared first on Kahawatungu.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Sat, 11 Jul 2026 01:55:19
Kupata huduma muhimu bado ni changamoto licha ya serikali kuanzisha vitengo vipya vya utawala 2023
LICHA ya serikali kuanzisha vitengo vipya vya utawala nchini tangu mwaka 2023 kwa lengo la kupeleka huduma karibu na wananchi, kuimarisha usalama na kuboresha uratibu wa shughuli za serikali, uchunguzi umebaini baadhi ya vitengo hivyo bado havijaanza kufanya kazi kikamilifu. Sababu kuu zinazochelewesha utekelezaji ni ukosefu wa fedha, kuchelewa kuajiri machifu na manaibu wao, pamoja na ukosefu wa ofisi na miundombinu muhimu. Maeneo yaliyoathirika zaidi ni Kaskazini Mashariki na Bonde la Ufa, ambako vitengo vingi vilianzishwa ili kukabiliana na changamoto za usalama. Katika eneo la Kaskazini Mashariki pekee, angalau tarafa saba, kata 26 na kata ndogo 38 bado havijaanza kutoa huduma. Kaunti ya Wajir inaongoza kwa kuwa na vitengo 40 visivyofanya kazi, ikifuatiwa na Garissa ikiwa na 19 na Mandera 12. Wakazi wanasema changamoto za usalama, migawanyiko ya koo na uhaba wa watumishi zimekwamisha utekelezaji. Garissa kwa mfano, baadhi ya wakazi bado husafiri zaidi ya kilomita 150 kupata huduma muhimu kama vitambulisho vya kitaifa na vyeti vya kuzaliwa. Kamishna wa Kanda ya Kaskazini Mashariki, Bw John Otieno, hata hivyo alisema mchakato unaendelea, akibainisha kuwa machifu na manaibu wao wanaendelea kuajiriwa huku manaibu wa makamishna wa kaunti tayari wakipelekwa katika maeneo mengi mapya. Kaunti ya Turkana imeonyesha mafanikio na changamoto kwa pamoja. Vitengo vipya kama Lokichogio, Aroo, Lokiriama na Suguta vimechangia kuimarisha usalama katika baadhi ya maeneo ya mpakani, ingawa wizi wa mifugo, ukosefu wa magari ya doria na barabara mbovu bado vikitatiza utoaji wa huduma. Katika mpaka wa Kenya na Sudan Kusini, wakazi wanasema hali ya amani imeimarika tangu kuanzishwa kwa vitengo hivyo mwaka 2024, huku kamati za amani na usimamizi wa rasilimali zikisaidia kuzuia migogoro. Katika Kaunti ya Kilifi, Tarafa ya Chasimba ndiyo pekee inayokaribia kuanza kufanya kazi kikamilifu, huku maeneo mengine kama Kitsoeni na Mwakambi yakiwa bado hayana machifu wala ofisi. Hali kama hiyo inashuhudiwa Taita Taveta ambako baadhi ya maeneo yanasubiri maafisa kupelekwa licha ya mahojiano kukamilika. Kaunti za Homa Bay na Kisumu pia zina vitengo vipya ambavyo bado haviwezi kutoa huduma zote za serikali kutokana na ukosefu wa watumishi na miundombinu. Wakazi wengi bado hulazimika kusafiri hadi makao makuu ya kaunti ndogo kupata huduma za usajili wa vitambulisho, vyeti vya kuzaliwa na huduma za polisi. Hata hivyo, Busia, baadhi ya wakazi wanasema vitengo vipya vimepunguza gharama na muda wa kupata huduma za serikali. Lakini katika maeneo jirani ya Mumias West, vituo vipya vya polisi bado havijaanza kufanya kazi licha ya fedha kutumika kujenga miundombinu hiyo. Huko Samburu, zaidi ya miezi sita baada ya kutangazwa kwa kaunti ndogo mpya, utekelezaji bado umekwama kutokana na ukosefu wa fedha.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Sat, 11 Jul 2026 01:38:03
How to Bold Text on WhatsApp
WhatsApp allows you to format your messages using simple text symbols, making it easy to emphasize important words or phrases. One of the most commonly used formatting options is bold text, which helps your messages stand out and improves readability. Learning how to bold text on WhatsApp can make your conversations clearer and more engaging [...] The post How to Bold Text on WhatsApp appeared first on Kahawatungu.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Sat, 11 Jul 2026 00:55:06
Ruto ajipigia debe akizindua awamu ya pili ya mpango wa Nyota
RAIS William Ruto Ijumaa alizindua rasmi awamu ya pili ya mpango wa kuwawezesha wafanyabiashara vijana (NYOTA), katika maeneo mbalimbali nchini kupitia mawaziri na maafisa wengine wakuu. Hatua hiyo ilionyesha mkakati mpya wa serikali wa kutumia mawaziri kufikisha sera na mipango yake moja kwa moja kwa wananchi huku ikipanua utekelezaji wa mpango huo wa kuwawezesha vijana. Rais Ruto aliongoza uzinduzi katika Uwanja wa Michezo wa Ulinzi jijini Nairobi, huku Naibu Rais Kithure Kindiki akiongoza shughuli za kaunti za Nakuru, Baringo na Nyandarua mjini Nakuru. Mkuu wa Mawaziri Waziri, Musalia Mudavadi aliongoza uzinduzi eneo la Magharibi uliohusisha Kakamega, Vihiga, Busia na Bungoma katika Chuo Kikuu cha Masinde Muliro. Naye Waziri wa Utumishi wa Umma, Geoffrey Ruku, aliongoza uzinduzi Meru, Embu na Tharaka Nithi mjini Chuka, huku Waziri wa Ardhi, Alice Wahome, akiongoza shughuli za kaunti za Nyeri, Kirinyaga na Murang'a. Waziri wa Kazi, Alfred Mutua alisimamia uzinduzi Machakos, Makueni na Kitui mjini Kitui. Shughuli kama hizo zilifanyika pia Nanyuki, Kapenguria, Eldoret, Bomet, Malindi, Mombasa, Kisumu, Kisii pamoja na Mandera, Wajir, Garissa na Marsabit. Ingawa alikuwa Nairobi, Rais Ruto alihutubia taifa kupitia matangazo ya moja kwa moja yaliyotangazwa katika vituo vyote vya uzinduzi, jambo lililoruhusu mawaziri na viongozi wengine kuwasilisha ujumbe mmoja wa kitaifa kwa wakati mmoja. Mpango huo unaolenga kuwawezesha vijana unatoa mtaji wa kuanzisha biashara, mafunzo ya ujasiriamali pamoja na ushauri wa kitaalamu ili kuwasaidia vijana kuanzisha na kukuza biashara zinazoweza kuzalisha ajira. Zaidi ya vijana 14,000 kutoka Nairobi, Kiambu na Kajiado walihudhuria uzinduzi huo jijini Nairobi, huku uzinduzi wa wakati mmoja ukiwawezesha vijana kutoka kaunti zote 47 kushiriki bila kulazimika kusafiri umbali mrefu. Serikali ilitenga Sh5.5 bilioni kufadhili vijana 110,000 wenye umri wa kati ya miaka 18 na 29 katika awamu ya kwanza ya mpango huo. Kwa jumla, NYOTA inatarajiwa kuwafikia takriban vijana 820,000 kupitia ufadhili wa biashara, ukuzaji wa ujuzi na fursa za ajira. "Tunataka kuhakikisha hakuna Mkenya anayeachwa nyuma. Zamani baadhi ya maeneo na wananchi walibaki nyuma, lakini sasa tumedhamiria kila Mkenya ajivunie nchi yake. Ndiyo maana mpango huu unatekelezwa katika wadi zote 1,450 nchini," alisema Rais Ruto. Alisema mpango huo umeundwa ili kuwapa vijana nafasi ya kushiriki katika ukuaji wa uchumi bila kujali kiwango cha elimu, hali ya kijamii au mwelekeo wao wa kisiasa. "Nataka kuwaambia vijana kuwa huu ni mpango wa vijana wenye umri wa miaka 18 hadi 29. Umeundwa kwa ajili ya vijana wa Kenya," alisema. Rais alisema walengwa wakuu ni vijana ambao kwa muda mrefu wamekosa mikopo kutoka taasisi za kifedha kutokana na ukosefu wa dhamana, mtaji au mitandao ya kibiashara. Alisisitiza kuwa uteuzi wa wanufaika utaongozwa na uwazi na uwajibikaji, wala si upendeleo wa kisiasa. "Hauhitaji kuwa gavana, chifu au mtu maarufu ili kufaidika. Mpango huu ni wa uwazi na uwajibikaji, na hautaendeshwa kwa misingi ya upendeleo," alisema. Aliwataka wanufaika kuripoti mtu yeyote atakayewaitisha fedha au kuwaelekeza kuunga mkono chama fulani cha kisiasa ili wapate nafasi katika mpango huo. "Huu si mpango wa kisiasa. Ni mpango wa biashara unaolenga kuwawezesha vijana," alisisitiza. Rais pia alisema hata vijana ambao hawakumaliza masomo ya sekondari au waliosoma hadi darasa la nane watapewa nafasi sawa. "Vijana wote ni Wakenya na serikali yetu ina wajibu wa kuwajali," alisema. Mbali na mtaji, wanufaika watapatiwa mafunzo ya biashara, ushauri na ufuatiliaji wa karibu ili kuhakikisha biashara zao zinakuwa endelevu. Hatutawapa fedha pekee. Tutawafunza, tutawashauri na tutatembea nanyi hadi mfanikiwe," alisema Rais. Kwa baadhi ya wanufaika, mpango huo tayari umeanza kubadili maisha yao. Kaunti ya Bungoma, Musembe alitumia fedha hizo kufungua duka la vifaa vya kielektroniki baada ya miaka mingi ya kukosa mtaji wa kununua bidhaa. Katika Kakamega, Sonya Wembo aliwekeza fedha hizo katika ufugaji wa kuku, akisema sasa ana nafasi ya kujenga biashara itakayomwezesha kujitegemea. Huko Kitui, Masoso Kituti alifungua bucha na anasema mtaji huo umempa fursa ya kujenga chanzo cha kudumu cha mapato. Garissa, Najma alipanua biashara yake kwa kuongeza bidhaa dukani, huku Kiprono wa Eldoret akiwekeza katika kilimo cha parachichi akisema ni uwekezaji wa muda mrefu utakaomletea kipato cha baadaye. Mbali na uzinduzi wa NYOTA, shughuli za Ijumaa zilionyesha jinsi serikali ya Kenya Kwanza inavyozidi kutumia mawaziri kueneza sera zake kote nchini kwa wakati mmoja badala ya kutegemea ziara za Rais pekee.
read morekenyans.co.ke
@kenyans Sat, 11 Jul 2026 00:45:03
Question Emerge After Iran State Media Warns Kenya Could Join U.S., Israel War
Despite the allegations, neither the Kenyan government nor the Nigerian government has issued an official response to the claims made by the leading Iranian broadcaster.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Fri, 10 Jul 2026 23:48:07
Boy killed in bomb explosion in Baringo
Police in Baringo County are investigating an incident in which a 15-year-old boy was killed after reportedly stepping on an abandoned explosive device in Tiaty West Sub-county. The incident occurred on Friday morning in the Toplen area of Silale Location. The victim was walking through the area when he allegedly stepped on what is suspected [...] The post Boy killed in bomb explosion in Baringo appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Fri, 10 Jul 2026 23:52:48
Man arrested on suspicion of murder after death of Ann Widdecombe
A 26-year-old man is being held on suspicion of murder following the death of former MP and government minister Ann Widdecombe. On Friday, Devon and Cornwall Police confirmed the man, a white British national, was arrested at an address in Newton Abbot, Devon and was is in custody. The body of the 78-year-old former Conservative [...] The post Man arrested on suspicion of murder after death of Ann Widdecombe appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Fri, 10 Jul 2026 23:55:51
Triple murder suspect arrested in South Africa
Police in South Africa say they have arrested a man on suspicion of murdering his wife and two daughters near Bedford. Nothabo Zandile Tshuma, 42, Natalie, 15, and Nala, five, were found dead at the family home in Great Denham on Monday. Zimbabwean national Ndodana Mkhanyisi Tshuma had left the country via Heathrow Airport on [...] The post Triple murder suspect arrested in South Africa appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Fri, 10 Jul 2026 23:58:44
US wants Iran to pledge to stop shooting at ships in Strait of Hormuz
The US wants Iran to publicly state that the Strait of Hormuz is open and to pledge to stop firing on commercial ships as part of negotiations due to be held on Saturday. US media cited unnamed officials as saying Tehran had privately acknowledged to President Donald Trumps advisers that the shooting at ships was [...] The post US wants Iran to pledge to stop shooting at ships in Strait of Hormuz appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Sat, 11 Jul 2026 00:01:36
KMTC mourns female student found dead at Nairobi campus
The Kenya Medical Training College (KMTC) announced the death of one of its students, Ann Odhiambo Adhiambo, whose body was discovered within the Nairobi Campus on July 7, 2026. Mystery surrounds her death amid murder investigations. Police believe she was killed as her body had injuries. The student died as a result of multiple internal [...] The post KMTC mourns female student found dead at Nairobi campus appeared first on Kahawatungu.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Fri, 10 Jul 2026 23:55:27
Wafanyabiashara Keumbu walilia hasara baada ya mkutano wa Linda Mwananchi kuvurugwa
WAFANYABIASHARA katika Soko la Keumbu, Kaunti ya Kisii, wanakabiliwa na wakati mgumu baada ya biashara yao kudorora kufuatia vurugu zilizotokea wakati wa mkutano wa kisiasa wa viongozi wa Linda Mwananchi Ijumaa iliyopita. Hali imezidi kuwa mbaya kutokana na kampeni kwenye mitandao ya kijamii inayowahimiza wananchi kususia bidhaa kutoka sokoni humo, kwa madai kwamba baadhi ya wafanyabiashara walihusika katika vurugu hizo. Ingawa hali ya usalama imeanza kutulia, wafanyabiashara wanasema idadi ya wateja imepungua kwa kiasi kikubwa na wengi wao sasa wanapata hasara. Bi Josephine Mang'ere alisema biashara ilikuwa ikiendelea vizuri kabla ya mkutano huo kuvurugika. "Tulikuwa tumewasubiri viongozi wa Linda Mwananchi, lakini baada ya muda mawe yakaanza kurushwa. Tangu siku hiyo biashara imekuwa ngumu. Tunapoenda kuuza bidhaa zetu watu hawazinunui. Tunaomba tusamehewe," alisema. Kwa upande wake, Bi Sophia Moraa alisema biashara yake ya parachichi imeathirika vibaya kwani wateja wengi wamekataa kununua mazao yake, hali iliyosababisha baadhi yake kuoza. "Sisi ni wafanyabiashara wasio na hatia. Tunapowafuata wateja barabarani wanatuambia tuuze bidhaa zetu kwa viongozi wanaotuhumiwa kusababisha vurugu. Tunataka siasa za amani," alisema. Bi Mary Moraa alisema wafanyabiashara sasa wanahimiza amani na kuheshimiana kisiasa. "Sisi ni wazazi. Kijana aliyefariki ni mtoto wetu pia, na kifo chake kinatuumiza. Wanasiasa wote waruhusiwe kuhutubia wananchi bila ubaguzi," alisema. Wakati huo huo, Meshack Yoge, mmoja wa manusura wa shambulizi dhidi ya msafara wa Linda Mwananchi, alisema anaamini alinusurika kifo kwa bahati. Bw Yoge, ambaye alijeruhiwa jicho baada ya kupigwa na jiwe, alisema tukio hilo lilikuwa la kutisha na bado hajapona kikamilifu. Alisema walikuwa wakielekea Keroka baada ya mkutano wa Kisii mjini na walipofika Keumbu, walivamiwa na kundi la watu waliokuwa wakirusha mawe na kubeba rungu, mishale na pinde. "Tuliona watu wakikimbia kuelekea kwetu wakipiga kelele wakisema, 'Waueni!' Dirisha la gari lilivunjwa, jiwe likanigonga usoni na kujeruhi jicho. Nilinusurika kupoteza jicho na meno," alisema. Aliongeza kuwa walilazimika kukimbia kwa kasi kuokoa maisha yao na baadaye akapelekwa hospitalini Keroka ambako alipatiwa matibabu. Mgombeaji wa udiwani wa Kisii Central, Bw Andrew Moindi Mochache, aliyekuwa ndani ya gari hilo, alisema waliona kifo wazi. "Niliona kifo kwa macho yangu. Watu waliotushambulia walikuwa wamekusudia kutuua," alisema. Kiongozi wa People's Liberation Party (PLP) Martha Karua na Mbunge wa North Mugirango Joash Nyamoko walilaani vurugu hizo, wakisisitiza kuwa siasa zinapaswa kuendeshwa kwa amani. Bi Karua alisema hakuna anayepaswa kuzuiwa kutoa maoni yake au kushiriki shughuli za kisiasa kwa amani, huku Bw Nyamoko akiwataka vijana kuepuka kutumiwa na wanasiasa kuchochea ghasia.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Fri, 10 Jul 2026 23:38:30
Amnesty calls latest US deportation to Eswatini 'unlawful'
Amnesty International criticised Friday the latest US deportation of 11 people to Eswatini as unlawful, accusing President Donald Trumps administration of cruel and racist anti-immigrant policies. The group was flown into the tiny African nation on Wednesday, the fourth batch to arrive since July last year as part of a $5-million deal with Washington. The [...] The post Amnesty calls latest US deportation to Eswatini unlawful appeared first on Kahawatungu.
read moreRight Column Content